Posts

Showing posts from October, 2018

Tazama fly over ya Tazara ilivyokimbiza ujenzi na huu ndio muonekano wake

Image
Leo August 2,2018 tunayo story kuhusu muonekano wa sasa wa barabara ya juu (Flyover) katika makutano ya barabara ya Nyerere na Mandela, eneo la TAZARA Jijini Dar es salaam. Barabara hii ya juu itakuwa ya kwanza hapa nchini na ujenzi wake umegharimu takribani Shilingi Bilioni 100 ambapo inatarajiwa kuzinduliwa September 2018 na Rais John Pombe Magufuli. Barabara hii itakuwa na njia 4 na urefu wa mita 300 kutokea maeneo ya katikati ya Jiji la Dar es salaam kuelekea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere na inatarajiwa kupunguza kero ya msongamano wa magari yaendayo na yatokayo Uwanja wa ndege na Bandari ya Dar es salaam. Kukamilika kwa ujenzi wa barabara hii kunatarajia kumaliza tatizo la msongamano wa magari Jijini Dar es salaam. Mbali ya barabara hii pia Dar es Salaam itakuwa na barabara nyingine za juu katika makutano ya barabara za Nelson Mandela, Morogoro na Sam Nojuma eneo la Ubungo.

Hakuna mwanaume rijali anayeweza kitaka wa na mwanamke mmoja

Image
Kwa wale nitakaowakwaza naomba mniwie radhi lakini kweli hata mimi hainipendezi kuyasema haya ila ni vema tu niwaeleze dada zangu kwasababu ukweli unaoumiza ni bora, kuliko uongo unaofurahisha. Hakuna mwanaume riijali anayeweza kuwa na mwanamke mmoja, eidha awe ameoa au hata kama hajaoa. Hakuna mwanaume wa aina hiyo Karne hii, usijidanganye kukimbilia kwenye ndoa ukiamini kwamba baada ya kuolewa utajimilikisha huyo mwanaume aliyekuoa, never. "Mchele mmoja mapishi mbalimbali", utakuta wewe mwanamke kila siku ukikutana na jamaa yako faragha lazima yeye ndio aombe kamchezo, wakati kuna sehemu akienda mwanamke mwenzako ndio anaandaa mazingira ya kuomba kamchezo kutoka kwa jamaa, now u see the difference. Mara zote mkitoka lazima wewe ndio uwe ume suggest mtoke tena yeye ndio ana pay bills, wakati kuna mwanamke mwenzio some where ingawa sio mara zote, ila mara chache chache yeye ndio anamuomba jamaa watoke na ndio ana pay bills, umeona. Humshauri jamaa hata kununua an asset,

Mwalimu mkuu auliwa kwa kuchomwa na kisu mbele ya Wanafunzi

Image
MWALIMU mkuu wa shule moja ya sekondari  Jumapili iliyopita alivamiwa na kundi la watu sita akiwa darasani akachomwa na kukatwakatwa kwa visu hadi kifo chake. Hili lilifanyika mbele ya wanafunzi wake 20 aliokuwa nao darasani katika shule inayojulikana kama Havanur Public School ya huko Bengaluru, Jimbo la Karnataka, India, polisi wamesema. Mmoja wa wauaji hao alikamatwa baadaye  na polisi katika eneo la Mahalaxmi Layout baada ya kudokezwa na raia wema.  Mtu huyo alijeruhiwa mguuni baada ya polisi kumrushia risasi kufuatia jaribio lake la kuwashambulia.  Baadaye mtu huyo alipelekwa hospitali. Mwalimu huyo aliyekuwa anaitwa Ranganath (60),  akiwa mwalimu mkuu wa shule hiyo iliyoko eneo la Agrahara Dasarahalli, alikuwa anaendesha masomo kwa wanafunzi wa darasa la kumi alipovamia na kundi hilo na kuuawa. Watu hao baadaye walitoroka katika gari dogo walilokuwa wemekwenda nalo shuleni hapo, walisema polisi. Polisi wanatuhumu mgogoro wa ardhi unaoihusisha shule hiyo kuwa ndiyo chanzo cha t

KUISHI UKWELI  WA MWALIMU

Image
LICHA ya Mwasisi wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere, kuwaacha Watanzania kwa takribani miongo miwili, maono yake mengi yanaendelea kuishi na kudumishwa na awamu ya tano. Hivyo hata kama Mwalimu angefufuka leo, akifurahia muendelezo wa maono yake na mafanikio makubwa yaliyofikiwa. Katika kumkumbuka Mwalimu. Nipashe, inazungumza na Mchumi na Mchambuzi wa masuala ya kijamii na maendeleo , Dk. Hoseana Lunogelo, kuangalia jinsi kazi za Mwalimu zinavyoakisiwa katika serikali  ya awamu  ya tano. Anaanza kwa kutaja baadhi ya mambo akisema mojawapo ya  kitu ambacho Nyerere alikiota ni suala la kila Mtanzania kupata elimu ili kufuta ujinga , kujiepusha na maradhi na kujiondoa kwenye umaskini. Anasema maono ya Mwalimu ya kuhakikisha kuwa kila Mtanzania anapata elimu yameendelea kuishi tena kwa kurejea sera ya elimu ya bure. Nyerere akiiongoza Tanzania kuanzia mwaka 1961 hadi 1985, alisimamia sera ya kutoa elimu bure kwa kila Mtanzania ili kila mmoja  asome.  Kwa kutumia rasilimali za umma

Ajira & Nafasi za Kazi kada ya Afya

Ajira Mpya kwa kada ya Afya awamu ya pili na Nafasi za Kazi kada ya Afya 05 October 2018 T A NGAZO LA KUITWA KAZINI.pdf KUONA MAJINA,BOFYA HAPA   AJIRA AWAMU YA PILI(REPLACEMENT).pdf Tangazo la nafasi za kazi  TANGAZO LA AJIRA REPLACEMENT.p KUOMBA AJIRA BOFYA HAPA   41.59.1.81

Jinsi Ya Kupata Fedha Zaidi Kutoka Kwa Mwajiri Wako

Image
Inabidi uwe makini kama unataka kulipwa zaidi Ingawa kampuni nyingi zinaongezea wafanyakazi wake mishahara kila mwaka, yapo makampuni mengi ambayo hayafanyi hivyo, hivo inabidi ufanye jitihada ili kupata ongezeko la mshahara. Lakini, mazungumzo kati yako na bosi wako kuhusu kuongezewa mshahara yanaweza kuwa jambo la kuogopesha.., hii pamoja na uoga wa kukataliwa hufanya wafanyakazi wengi wasijaribu kufanya hivyo. Lakini, kumbuka kuwa, usipojitetea utabaki na mshahara ule ule paka utakapo pandishwa cheo au kuhamia kampuni nyingine. Hivyo uwezo wa kuongea na bosi wako kwa ujasiri kuhusu ongezeko la mshahara ni maarifa muhimu ambayo yatakusaidia kwenye soko la ajira. Je, unatakiwa ufanye nini hasa? Jua thamani yako katika soko la ajira Ingawa unaweza kufikiri kuwa unastahili fedha nyingi zaidi ya unazopokea sasa, ongezeko la mshahara unalotaka lazima liwe na sababu. Kwa mfano kama watu wengi katika taaluma yako ambao wana uzoefu sawa wanapokea TZS 2,000,000 kwa mwezi, hala

MAISHA NA MAFANIKIO

BAADHI YA MISEMO NA METHALI TOKA TANZANIA 1. Acha kukuna makovu ya mende (Kichaga) Maana yake ni kwamba uache kukumbuka taabu ya wakati uliopita. Methali hii itafahamika vizuri kama tukielewa kwamba hapo zamani katika jamii zetu, mende walikuwa wanaonekana kwa wingi katika nyumba. Nao mende ni hodari wa kuuma watu wakati wa usiku wakiwa wamelala. Na pale walipouma hubaki kovu ambalo hukuna. Lakini pia ambaye ameshaumwa na mende hao itakuwa ni kazi bure kama atakalia kuyakuna makovu hayo. Methali hii hutumika kwa kuwaonya watu wasikalie kufikiria makosa au taabu za wakati uliopita. 2. Afadhali kuchakaza nguo kuliko akili(Kipare) Maana yake ni kuwa hakuna kitu bora kama akili (hekima). Mtu ambaye hana hekima ya uchi kuliko uchi wa aina yoyote ile. Kuwa uchi kinguo, mtu anaweza kununua zingine. Lakini mtu anapokuwa uchi kiakili, hakuna maarifa. Methali hii hutumika kwa kumhurumia mtu ambaye ameharibikiwa na akili na anafanya majambo isivyotakiwa katika jamii. 3. Amekufa hata