Posts

Showing posts from March, 2018

Tetesi za Soka Ulaya Jumamosi 24.03.2018

Image
Image caption Neymar huenda akaikosa michuano ya kombe la dunia kwa kuwa majeruhi Manchester City na Manchester United zote kwa pamoja zitapambana kujaribu kumsajili nyota wa Brazil Neymar iwapo ataamua kuondoka Paris St-Germain. Real Madrid pia wanajaribu kupata saini yake, lakini PSG wamesema hawamuachii. (Mundo Deportivo - in Spanish) Kufuatia kocha wa Manchester Jose Mourinho kumshambulia kwa maneno mlinzi wa kushoto wa klabu hiyo Luke Shaw, kunaweka pia hatarini kumpata winga wa Real Madrid na raia wa Wales Gareth Bale. (mail) Gareth Bale ataondoka Real Madrid na kujiunga na Manchester United wakati wa majira ya joto iwapo Zinedine Zidane atasalia kuiongoza miamba hiyo ya Bernabeu .(mirror) Lakini mshambuliaji huyo wa Real Madrid, ameambiwa na meneja wa Wales na kiungo wa zamani wa Manchester United Ryan Giggs kusalia katika La Liga kuliko kurudi Premier League. (express) Image caption Rashford ataiongoza Uingereza kwenye safu ya ushambuliaji katika michuano ya kombe la

Mimea sita yenye sifa za kushangaza zaidi duniani

Image
Haki miliki ya picha AFP/GETTY Image caption Mmea huu hutoa harufu ya mzoga Duniani huwa kuna mimea ya aina nyingi, lakini kunayo baadhi ambayo inashangaza kwa sifa zake za kipekee. Hapa, tutaangazia sita kati ya mimea hiyo na kukueleza ni kwa nini ni ya kushangaza. Ua la Mauti Ndio mmea unaochanua maua makubwa zaidi duniani. Kwa kisayansi mmea huo hufahamika kama Haki miliki ya picha AFP/GETTY Image caption Ua la Mauti huwa kubwa sana Rafflesia arnoldii na hukua kwenye misitu yenye mvua nyingi maeneo ya Sumatra na Borneo. Ukiutazama unaweza kudhani ni mmea kutoka sayari nyingine. Nabii kutoka Malawi anayedai kutenda miujiza Ua lake linaweza kuwa na upana wa mita moja. Mmea huu huwa hauna majani, miziz au shina. Mmea huu hupata virutubisho na maji kwa kuinyonya mimea mingine. Ua la mmea huu huvunda sana, hutoa harufu sawa na ya mzoga. Ndio maana huitwa Ua la Mauti. Mmea huu huvutia wadudu wa kusaidia katika kuchavusha. Bingwa wa kukua haraka Haki miliki ya picha AF

Umoja na amani ya Tanzania viko hatarini;Maaskofu wa kilutheri waonya

Image
Haki miliki ya picha GETTY IMAGES Image caption Baraza la maaskofu wa kanisa la Kiinjili la Kilutheri chini Tanzania (KKKT) limetoa waraka maalum wa Pasaka Baraza la maaskofu wa kanisa la Kiinjili la Kilutheri chini Tanzania (KKKT) linasema umoja na amani ya Tanzania viko hatarini. Katika waraka wa ujumbe wa pasaka unaosambaa katika mitandao ya kijamii na kutarajiwa kusomwa kesho katika makanisa mbali mbali ya KKKT nchini Tanzania, baraza hilo limeorodhesha mambo kadhaa ambayo wameyataja kuwa ndio tishio la umoja na amani ya nchi hiyo. Waraka umeyataja baadhi ya mambo hayo kuwa ni pamoja na utekaji, utesaji, kupotea kwa watu, mashambulizi ya silaha dhidi ya viongozi wa kisiasa, mauaji yenye mwelekeo wa kiitikadi, vitisho, ubambikiziaji wa kesi, na matumizi mabaya ya vyombo vya dola dhidi ya wananchi. "Kukosekana kwa mazingira ya haki na uhuru wa kuchagua na kuchaguliwa katika chaguzi mbalimbali. Chaguzi zote zimeghubikwa na ubabe, vurugu, hila, na vitisho", imeso

Xdolls: Vyumba vya midoli ya mapenzi vinavyozua mjadala Paris vyanusurika

Image
Haki miliki ya picha GETTY IMAGES Image caption Mmiliki wa Xdolls amesema midoli yake ni sawa na vifaa vingine vya kujitosheleza kimapenzi Madiwani katika jiji la Paris wametupilia mbali hoja ambayo ililenga kufunga biashara ambayo imekuwa ikihusisha watu kulipia kukaa na midoli ya mapenzi kwa saa moja. Wateja hulipishwa €89 ($109; £78) kukaa na midoli hiyo iliyotengenezwa kwa madini ya silicone. Madiwani wa chama cha Kikomunisti pamoja na watetezi wa haki za wanawake walikuwa wameliomba Baraza la Jiji la Paris ambalo huhusika katika kusimamia jiji hilo kujadili uwezekano wa kufunga biashara hiyo ambayo imekuwa ikifahamika kama Xdolls. Wamekuwa wakisema biashara hiyo inadhalilisha wanawake na kimsingi ni kama danguro. Ni haramu kumiliki au kuendesha biashara ya danguro nchini Ufaransa. Lakini polisi walifika katika biashara hiyo kabla ya mkutano wa baraza hilo la jiji kufanyika na wakatangaza kwamba hakuna sheria zozote zilizokuwa zimevunjwa. Katika taarifa ya pamoja, madi

Wafanyakazi wapenda kazi kupita kiasi kufukuzwa wakapumzike Korea Kusini

Image
Haki miliki ya picha ISTOCK Image caption Korea Kusini ina utamaduni wa watu kufanya kazi muda wa ziada sana Serikali nchini Korea Kusini imeanzisha mpango wa kuwalazimisha wafanyakazi kuondoka kwa wakati baada ya kumalizika kwa zamu yao. Mpango huo unahusisha kuzimwa kwa lazima kwa kompyuta za wafanyakazi hao ofisini saa mbili usiku kila Ijumaa. Lengo la mpango huo ni kujaribu kufikisha kikomo "utamaduni wa kufanyakazi muda wa ziada". Wafanyakazi nchini humo hufanya kazi muda mwingi zaidi kwa siku ukilinganisha na wafanyakazi wengine nchi nyingine duniani. Wafanyakazi wa serikali Korea Kusini kwa kawaida hufanya kazi saa 2,739, muda ambao ni saa 1,000 zaidi ya muda wanaofanya kazi watumishi wa umma katika mataifa yaliyoendelea. Kwa Picha: Treni yenye starehe na ghali yaundwa Japan Siku ambayo BBC ilikosa habari Matukio 10 makuu mwongo mmoja wa iPhone Mpango huo wa kuzima kompyuta kwa lazima utaanza kutekelezwa na serikali ya jiji la Seoul kwa awamu tatu k