Posts

Showing posts from April, 2018

Liverpool yatinga nusu Fainali

Image
Haki miliki ya picha GETTY IMAGES Image caption Furaha ya ushindi ya wana Liverpool Liverpool imefika katika nusu fainali yao ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa kwa miaka 10 baada ya kujikokota na kuishinda Manchester City kwa kupata ushindi wa mabao 2-1 yaliyoleta ushindi wa jumla wa Liverpool 5-1 Man City. City walianza vizuri wakati walipojaribu kulipa deni la 3-0 walizofungwa katika mechi ya kwanza. Ilikuwa dakika ya pili tu ya mchezo ambapo Raheem Sterling alimwanzishia Gabriel Jesus aliyeitumia nafasi hiyo kupachika bao la kuwapa matumaini Man City. Hata hivyo baada ya tukio la vurugu kabla ya muda wa mapumziko lililoisha kwa Meneja Pep Guardiola kuondoshwa katika eneo la benchi la ufundi, City hawakuweza kuyafikia matamanio yao. Tukio lenyewe lilianzia pale ambapo Bernardo Silva alikuwa amepiga mkwaju kuelekea lango la Liverpool, huku Liverpool ikiwa katika shinikizo zito, mpira ukamkuta Leroy Sane ambaye aliukwamisha wavuni na kuwafanya City kudhani wamefanikiwa kupata goli la

Roma yalipa deni la Barca, yatinga nusu fainali

Image
Haki miliki ya picha REUTERS Image caption Wachezaji wa zamani wa timu ya Manchester City , Edin Dzeko and Aleksandar Kolarov, wakishangilia ushindi juu ya wenzao wa timu ya Roma wakati timu yao ya zamani ikitolewa Roma imefanya maajabu baada ya kuwabamiza Barcelona 3-0 na hivyo kutinga nusu fainali za mabingwa Ulaya kwa faida ya goli la ugenini. Barca walikuwa wanapewa nafasi kubwa ya kusonga mbele kutokana na kuingia uwanjani wakiwa na akiba ya magoli, ambapo kutokana na mechi ya kwanza waliyoipiga Roma bao 4-1, Roma ilikuwa inalazimika kuifunga Barcelona 3-0. Goli la Edin Dzeko dakika za awali za mchezo (6'), na Penalty ya Daniele de Rossi katika kipindi cha pili dakika ya 58 yamekamilishwa na Goli la Mlinzi Kostas Manolas alilofunga zikiwa zimesalia dakika nane tu mechi kufikia mwisho zimewafanya Barcelona pamoja nakuwa na Lionell Messi ambaye hakufurukuta, kuondokakichwa chini katika Ligi ya mabingwa barani Ulaya. Umati uliokuwepo Stadio Olimpico ulilipuka mara baada ya

Mambo 6 ya kutegemea Zuckerberg atakapotoa ushahidi kwa mabaraza ya Congress

Image
Haki miliki ya picha REUTERS Image caption Bwana Zuckerberg atakabiliana na hoja kali kuoka kwa mabunge yote mawili ya Marekani kuhusu taarifa/ data za kibinafsi hususan zile zinazolenga sakata la Cambridge Analytica Mark Zuckerberg amekuwa akijiandaa kwa jaribio lake kubwa huku Mkurugenzi mkuu huyo wa Facebook - akikabiliwa na maswali kutoka kwa mabaraza yote mawili ya congress Baadhi wanaonelea vikao hivi viwili kama zaidi ya mchezo wa kisiasa wa kuigiza , kama ni fursa ya wanasiasa kuonekana kwente Ttelevisheni wakimkosoa kwa ukali mtu tajiri na mwenye mamlaka. Huenda kukawa na ukweli katika hili. Lakini ni dhahiri kwamba haijawahi kutokea nafasi ya kumchambua Zuckerberg ambaye hapatikani kwa urahisi kutokana na kulindwa na kufichwa na kikosi chake cha maafisa wa mahusiano ya ummapamoja na manaibu wake. Taarifa yake ya ufunguzi wa iliyoandaliwa tayari imetolewa. Zuckerberg aahidi kurekebisha Facebook Facebook kufanya mabadiliko makubwa Lakini vikao hivyo vya mabunge maw

Trump aapa ''kutumia nguvu'' kujibu shambulio ''la kemikali'' Syria

Image
Image caption Rais Donald Trump amesema Marekani inapata ''msaada mzuri" juu ya nani aliyehusika na shambulio la Douma Jumamosi. Rais wa Marekani Donald Trump ameahidi " kutumia nguvu " kujibu madai ya shambulio la kemikali nchini Syria, huku mataifa ya magharibi yakitafakari hatua watakayoichukua. "Tuna njia nyingi za kijeshi,"aliwambia waandishi wa habari. Aliongeza kuwa hatua ya kujibu shambulio hilo itaamuliwa katika kipindi cha "muda mfupi". Bwana Trump alisema kuwa Marekani inapata ''msaada mzuri" juu ya nani aliyehusika na shambulio la Douma Jumamosi. Duru za kitabibu zinasema makumi kadhaa ya watu waliawa katika shambulio hilo, lakini idadi kamili haijathibitishwa. Bw Trump pia alijadili tukio hilo la rais wa Ufaransa Emmanuel Macron Jumatatu jioni, na viongozi wote walielezea utashi wao wa "kujibu kikamilifu". Image caption Mjumbe wa Marekani Nikki Haley alisema kuwa-wanaounga mkono jeshi la Syrian -

Mkuu wa zamani wa majeshi Sudan Kusini aunda vugu vugu jipya la waasi

Image
Haki miliki ya picha REUTERS Image caption Raia wa Sudan ya kusini Aliyekuwa Mkuu Majeshi Sudan Kusini ameunda vugu vugu jipya la kundi la waasi. Paul Malong ambaye alitimuliwa katika wadhifa wake na Rais Salva Kiir mwaka, amechukua hatua hiyo wakati nchi yake ikianza tena mazungumzoa ya amani mjini Addis Abba Ethiopia. Mazungumzo hayo pia, yana lenga kufikia makubaliano ya kuachiliwa kwa Makamu Rais Riek Machar ambaye kwa sasa yuko katika kizuizi cha nyumbani nchini Afrika Kusini. Malong amekuwa akiishutumu serikali kwa rushwa na makosa ya kuifilisi nchi, anasema kuwa kundi lake la waasi litakuwa na jukumu kubwa la kuiondoa Sudan Kusini kwenye sintofahamu na kuielekeza katika demokrasia na maendeleo. Sudan Kusini yaonywa kukumbwa na maafa Wasanii Sudan kusini wachora kushinikiza amani Haki miliki ya picha REUTERS Kufuatia kuundwa kwa kundi jipya la waasi, serikali ya Suda Kusin haijasema neno lolote, ambayo inapigana na vikundi kadhaa vya waasi nchini mwake . Inaarifi

Mark Zuckerberg akiri kampuni yake inakabiliana na Urusi

Image
Image caption Mtendaji mkuu wa mtandao wa kijamii Facebook, Mark Zuckerberg Mmiliki wa Facebook amewaambia maseneta wa Marekani kuwa kampuni yake imekuwa ikipambana na watumiaji wa Warusi wanaotaka kuutumia vibaya mtandao huo wa kijamii " Haya ni makabiliano ya kijeshi. Watarekebika ,"alisema he said. Bw Zuckerberg alikua akijibu maswali kuhusiana na sakata ya matumizi mabaya ya data za kibinafsi maarufu kama Cambridge Analytica. Pia amefichua kuwa Robert Mueller, kutoka baraza maalum linalochunguza madai ya Urusi kuingilia uchaguzi wa Marekani wa Mwaka 2016 aliwahoji wafanyakazi wa Facebook. Haki miliki ya picha GETTY IMAGES Image caption Bw Zuckerberg amesema kuwa kampuni yake sasa imetengeneza nyenzo za kubaini akaunti gushi Bwn Zuckerberg yeye hakuwa miongoni mwa watu waliohojiwa na ofisi ya Bw Mueller Lakini aliongeza kuwa : "kazi yetu na baraza maalum ni ya siri na ninataka kuhakikisha kwamba katika kikao cha wazi sifichui chochcote juu ya taarifa za sir