Posts

Showing posts from March, 2019

Sheria 17 za mpira wa miguu, Soka

Kila msimu mpya, Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) hutoa mabadiliko ya “Sheria za Mchezo” zinazoelezea kiundani taratibu za mchezo huo. Zifuatazo ni Sheria 17 za mpira wa miguu. Sheria #1: Uwanja Kuna vipimo maalumu vya viwanja wa mchezo wa soka, viwanja vidogo na vikubwa kadhalika. FIFA inasema kwamba katika mashindano ya mchezo wa soka wenye timu za wachezaji 11 kila moja, urefu wa uwanja unatakiwa uwe kati ya mita 100 na mita 130 na upana wake uwe kati ya mita 50 na 100. Kuna nafasi 11 za wachezaji kwenye uwanja wa mpira wa miguu lakini zote zinaweza kuwekwa kwenye makundi makuu manne. Kwenye michezo midogo, idadi ya wachezaji kwenye kila timu inaweza kupungua lakini nafasi hizi zinabaki kama zilivyo. Nafasi hizi kwenye mchezo wa soka ni Golikipa, safu ya ulinzi, viungo na washambuliaji. Sheria #2: Vipimo vya mpira Mzingo (mzunguko) wa mpira wa miguu hautakiwi kuzidi kipimo cha inchi 28 (sawa na sentimita 70) na hautakiwi kupungua inchi 27 (sawa na sentimita 68). Mpira saizi namba 5

Mabadiliko ya Kanuni za Mpira wa Miguu kwa Msimu wa 2019/2020

Image
The International Football Association Board (The IFAB) , imebadilisha baadhi ya kanuni za mchezo wa soka kwenye kikao kilichofanyika wiki iliyopita nchini Scotland . Mabadiliko hayo ni kama ifuatavyo:- 1. KUTAKUWA HAKUNA MREJESHO KUTOKANA NA PIGO LA PENATI Mchezo utasimama kwa kuanzishwa kama penati imeokolewa au imegonga mwamba , hii ina maana hakuna tena nafasi ya kufuata mpira na kufunga ( Rebound ) kwa maana hiyo wachezaji hawatokuwa na uhitaji wa kujipanga nje ya 18. 2.MPIRA KUCHEZWA NA MKONO. Kuanzia Juni mosi goli litakalofungwa ambalo limegusa mkono wa mchezaji kwa maksudi au bahati mbaya ( Mfungaji ) halitakubaliwa. 3.MABADILIKO YA MCHEZAJI  Mchezaji ambaye atakuwa anafanyiwa mabadiliko ataruhusiwa kutoka kupitia upande wowote ule wa uwanja  4. GOAL KICK  Mchezaji ataruhusiwa kugusa mpira hata ndani ya eneo la 18 kutoka kwa kipa , ambapo sasa hivi ni mpaka mpira utoke kwenye 18 ndio unaruhusiwa kuugusa. 5. KADI KWA MAKOCHA. Makocha sasa nao watakuwa wanaoneshwa kadi ya njano

TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA ZA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI, FEBRUARI 2019

Image
J AMHU R I YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA R AIS - TAMISEMI TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA ZA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI, FEBRUARI 2019 Ofisi ya Rais - TAMISEMI inapenda kuutangazia Umma kuwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa John Pombe Joseph Magufuli, anaendelea na kuongeza idadi ya watumishi katika Sekta ya Umma kwa kutoa nafasi nyingine za ajira kwa vijana wa Kitanzania katika Sekta ya Elimu. Mchakato huu wa sasa wa ajira utahusisha ajira mpya za watumishi 4549. Ajira hizi zitahusisha walimu wa Shule za Msingi na Sekondari. Kwa sababu hiyo, OR-TAMISEMI inawatangazia walimu wenye sifa kutuma maombi yao kwa njia ya mtandao kupitia kiunganishi cha http://ajira.tamisemi.go.tz ( Online Teacher Employment Application System – OTEAS). Walimu wanaotakiwa kutuma maombi ni wenye sifa za kitaaluma kama ifuatavyo: A.               WALIMU WATAKAOAJIRIWA SHULE ZA MSINGI i.           Mwalimu Daraja la IIIA -