Mark Zuckerberg akiri kampuni yake inakabiliana na Urusi

news
Image captionMtendaji mkuu wa mtandao wa kijamii Facebook, Mark Zuckerberg
Mmiliki wa Facebook amewaambia maseneta wa Marekani kuwa kampuni yake imekuwa ikipambana na watumiaji wa Warusi wanaotaka kuutumia vibaya mtandao huo wa kijamii
" Haya ni makabiliano ya kijeshi. Watarekebika ,"alisema he said.
Bw Zuckerberg alikua akijibu maswali kuhusiana na sakata ya matumizi mabaya ya data za kibinafsi maarufu kama Cambridge Analytica.
Pia amefichua kuwa Robert Mueller, kutoka baraza maalum linalochunguza madai ya Urusi kuingilia uchaguzi wa Marekani wa Mwaka 2016 aliwahoji wafanyakazi wa Facebook.
Nembo ya FacebookHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionBw Zuckerberg amesema kuwa kampuni yake sasa imetengeneza nyenzo za kubaini akaunti gushi
Bwn Zuckerberg yeye hakuwa miongoni mwa watu waliohojiwa na ofisi ya Bw Mueller
Lakini aliongeza kuwa : "kazi yetu na baraza maalum ni ya siri na ninataka kuhakikisha kwamba katika kikao cha wazi sifichui chochcote juu ya taarifa za siri.
Mwezi Februari, Ofisi ya Bw Mueller ilishtakiwa na Warusi 13 kwa kudukua taarifa za uchaguzi wa mwaka 2016, pamoja na makampuni matatu ya Urusi.
utokana na hojaji hiyo hisa za mtandao wa Facebook jana ziliongezeka mpaka kufikia asilimia nne
Image captionKutokana na kuhojiwa kwa Bw Zuckerberg na seneti ya Marekani hisa za mtandao wa Facebook jana ziliongezeka hadi kufikia asilimia nne
Bw Zuckerberg amesema kuwa kampuni yake sasa imetengeneza nyenzo za kubaini akaunti gushi.
Awali Mtendaji mkuu wa mtandao wa kijamii Facebook, Mark Zuckerberg ameomba msamaha kwa kamati ya Seneti ya Marekani kwa kuruhusu makampuni kadhaa kutumia vibaya data binafsi za jukwaa hilo kisiasa.
Mark Zuckerberg alijitetea kwa muda wa saa tano katika jopo la wasikilizaji kutoka bunge la seneti la Marekani linalohusika na masuala ya biashara na kamati ya mahakama.
Wakati wa hoja dhidi yakeBw Zuckerberg pia alisema:
  • "Ni wazi sasa kwamba hatukufanya juhusi za kutosha kulinda nyenzo zetu dhidi yakutumiwa kwa madhara"
  • "Ukiangalia mambo yalivyokwenda yalikuwa ni makosa ya wazi" kuamini kuwa Cambridge Analytica ilifuta data, bila kufanya uchunguzi zaidi
  • Hahisi "kama " Facebook ina udhibiti
  • Kwamba wakati wote kutakuwa na kitengo kisicholipiwa cha Facebook, kunachoweza kulipiwa , kitengo ambacho hakina matangazo ya biashara cha mtandao wa kijamii
  • Kukabiliana na kauli za uchochezi wa chuki " una kiwango cha juu cha makosa kuliko vile ninavyotaka "
  • Binafsi alihofia juu ya uwezekano wa upendeleo wa kisiasa kwneye kampuni yake
Mark ZuckerbergHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionKinyume na matarajio ya ulimwengu, wakati wa kikao dhidi yake badala ya kuvaa fulana kama alivyozoeleka, Bw Zuckerberg alikuwa maevalia nadhifu suti nyeusi
Kutokana na hojaji hiyo hisa za mtandao wa Facebook jana ziliongezeka mpaka kufikia asilimia nne , nao wanasheria nchini Uingereza na Marekani wameanzisha mashtaka dhidi ya Facebook, Cambridge Analytica, na makampuni mengine mawili yanayounganishwa na kesi hiyo.
Na baada ya utetezi wake Mark ameelezea hisia zake kutokana na mtandao wa Facebook hapa ulipofikia na yanayojiri hafurahishwi na chochote.
Utetezi wa Mark Zuckerberg, umepokelewa vyema na masoko ya hisa na hivyo kuifaidia Facebook kwa ongezeko la hisa asilimia nne unusu.

Comments

Popular posts from this blog

FAIDA ZIPATIKANAZO KWA KUTUMIA TUNGUJA PORI,NYANYA ZA MSHUMAA/CHUNGU/NGOGWE KIAFYA.

DALILI YA KUZIDI ASIDI MWILINI YOUR BODY IS ACIDIC HERE IS WHAT YOU NEED TO DO (THE REAL TRUTH BEHIND CANCER)

FAIDA YA MBOGA YA MCHICHA NI DAWA YA KUTIBU MARADHI MENGI TU UKITUMIA.