TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA WIZARA YA AFYA


Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR - TAMISEMI) imepata kibali cha ajira mbadala chenye Kumb Na. FA 97/128/01/”A’’/31 cha tarehe 12 Julai 2019 kwa ajili ya kuajiri watumishi 550 wa kada mbalimbali za afya. Hivyo, Ofisi ya Rais, TAMISEMI inapenda kuwatangazia wahitimu wote wa kada za Afya nchini kuwasilisha maombi ya nafasi za kazi, kuanzia leo tarehe 22/07/2019 ili kujaza nafasi mbalimbali za Kada ya Afya katika Hospitali za Wilaya, Vituo vya Afya na Zahanati.
Nafasi zinazotangazwa ni zifuatazo:- 

1. Daktari Daraja la II Waombaji wawe na Shahada ya Udaktari wa binadamu kutoka Vyuo Vikuu/Vyuo vinavyotambuliwa na Serikali waliomaliza mafunzo ya kazi “Internship” ya muda usiopungua mwaka mmoja na kupata usajili kutoka Baraza la Madaktari Tanganyika (Medical Council of Tanganyika). 
2. Tabibu Daraja la II Waombaji wawe na Stashahada (Diploma) ya Utabibu ya muda wa miaka mitatu kutoka Chuo kinachotambuliwa na Serikali. 
3. Tabibu Msaidizi Waombaji wawe wamehitimu Astashahada ya miaka miwili ya Tabibu Wasaidizi (Clinical Assistants Certificate) kutoka Chuo kinachotambuliwa na Serikali. 
 4. Afisa Muuguzi Daraja la II Waombaji wawe na Shahada ya Uuguzi kutoka Chuo Kikuu kinachotambuliwa na Serikali, waliohitimu mafunzo ya vitendo kazini (Internship) ya mwaka mmoja, waliosajiliwa na Baraza la Wauguzi na Wakunga Tanzania.
 5. Afisa Muuguzi Msaidizi Daraja la II Waombaji wawe na Stashahada (Diploma) ya Uuguzi ya muda usiopungua miaka miwili kutoka Chuo kinachotambuliwa na Serikali, waliosajiliwa na Baraza la Wauguzi na Wakunga Tanzania. 
6. Muuguzi Daraja la II Waombaji wawe na Cheti cha Uuguzi cha miaka miwili kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali na kusajiliwa (Enrolled) na Baraza la Wauguzi na Wakunga Tanzania. 
7. Afisa Afya Mazingira Daraja la II Waombaji wawe na Shahada ya Sayansi ya Afya ya Mazingira na mafunzo kazini na kusajiliwa na Bodi ya Wataalam wa Afya ya Mazingira. 
8. Afisa Afya Mazingira Msaidizi Daraja la II Waombaji wawe na Stashahada ya Sayansi ya Afya ya Mazingira ya miaka mitatu kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali na kusajiliwa na Bodi ya Wataalam wa Afya Mazingira. 
9. Mteknolojia Daraja la II (Maabara) Waombaji wawe na Stashahada (Diploma) ya Sayansi ya Maabara ya muda wa miaka mitatu kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali na kusajiliwa na Mabaraza ya Taaluma. 
10.Mteknolojia Msaidizi (Maabara) Waombaji wawe wamehitimu Astashahada ya miaka miwili katika fani ya Maabara kutoka Chuo kinachotambuliwa na Serikali na ambao wamesajiliwa na Mabaraza yao pale inapohusika.  
11.Mteknolojia Daraja la II (Mionzi) Waombaji wawe na Stashahada (Diploma) ya Sayansi ya Mionzi ya muda wa miaka mitatu kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali na kusajiliwa na Mabaraza ya Taaluma. 12.Mteknolojia Daraja la II (Dawa) Waombaji wawe na Stashahada (Diploma) ya Sayansi ya Dawa ya muda wa miaka mitatu kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali na kusajiliwa na Mabaraza ya Taaluma. 
13.Mtoa Tiba kwa Vitendo Daraja la II Waombaji wawe na Stashahada ya miaka mitatu (Diploma) katika fani ya Fiziotherapia/ Mtoa Tiba kwa Vitendo kutoka Chuo kinachotambuliwa na Serikali. 

14.Msaidizi wa Afya (Mhudumu wa Afya) Waombaji wawe wahitimu wa kidato cha nne waliopata mafunzo ya Mwaka mmoja katika fani ya afya katika chuo kinachotambuliwa na Serikali.

 SIFA ZA MWOMBAJI;
 i. Awe raia wa Tanzania; ii. Awe na umri usiozidi miaka 45; iii. Asiwe Mwajiriwa wa Serikali au asiwe Mwajiriwa wa Hospitali za Mashirika ya Dini ambaye mshahara wake unalipwa na Serikali; iv. Asiwe amewahi kuajiriwa Serikalini; v. Asiwe na check namba, na endapo itabainika kuwa aliwahi kuajiriwa Serikalini, atatakiwa kuzingatia utaratibu wa uhamisho au kurejea katika Utumishi wa Umma baada ya kuacha kazi kama ilivyobainishwa kwenye Waraka Na. CCB 228/271/01 wa tarehe 07 Agost, 2012.

 MAOMBI YOTE YAAMBATANISHWE NA;
 i. Nakala ya cheti cha kidato cha nne/sita; ii. Nakala za Vyeti vya Taaluma; iii. Nakala ya cheti cha kuzaliwa; iv. Nakala ya cheti cha usajili kamili (Full Registration) au Leseni ya kufanya kazi ya taaluma husika; 4 v. Maelezo binafsi (CV); na vi. Waombaji wanaojitolea na wale wanaomaliza muda wa ajira za mikataba kutoka kwa Wadau wa Maendeleo katika Sekta ya Afya wanatakiwa kuambatanisha barua za uthibitisho kutoka kwa Wakurugenzi wa Halmashauri husika.

 MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KWA WAOMBAJI WOTE
 i. Waombaji wote wawe tayari kufanya kazi Halmashauri yoyote watakayopangiwa; ii. Waombaji wote wawe tayari kufanya kazi na mashirika/taasisi zilizoingia ubia na Serikali; iii. Waombaji waliosoma nje ya nchi wanatakiwa waambatanishe pamoja na equivalent certificate kutoka NECTA/NACTE/TCU; na iv. Waombaji watakaotuma/waliotuma maombi yao ya kazi Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto hawapaswi kuomba nafasi hizi za kazi za Ofisi ya Rais, TAMISEMI.

 Maombi yote yatumwe kwa njia ya mtandao (online) kupitia mfumo wa kielektroniki unaopatikana kupitia anuani ya ajira.tamisemi.go.tz. Maombi yoyote yatakayowasilishwa kwa njia ya posta au kuletwa moja kwa moja Ofisini hayatafanyiwa kazi. Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 05 Agosti, 2019 saa 9:30 alasiri. Tangazo hili linapatikana katika tovuti yetu www.tamisemi.go.tz Limetolewa na: Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mji wa Serikali – Mtumba, S.L.P 1923, DODOMA. 22 Julai, 2019
Click here to start application
http://ajira.tamisemi.go.tz

Comments

Popular posts from this blog

FAIDA ZIPATIKANAZO KWA KUTUMIA TUNGUJA PORI,NYANYA ZA MSHUMAA/CHUNGU/NGOGWE KIAFYA.

DALILI YA KUZIDI ASIDI MWILINI YOUR BODY IS ACIDIC HERE IS WHAT YOU NEED TO DO (THE REAL TRUTH BEHIND CANCER)

FAIDA YA MBOGA YA MCHICHA NI DAWA YA KUTIBU MARADHI MENGI TU UKITUMIA.